KOCHA wa Juventus, Massimiliano Allegri amerejesha wimbi la ushindi San Siro baada ya jana kushinda bao 1-0 dhidi ya AC Milan katika Serie A.
Shukrani kwake mfungaji wa bao hilo pekee, Carlos Tevez aliyeizima AC Milan na kumpa raja kocha huyo ambaye Juve ilimfukuza miezi nane iliyopita.
Tevez, aliyefunga mabao yote Jumanne wakati Juve ikishinda 2-0 katika Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Malmo, alifunga bao hilo baada ya ushirikiano mzuri na Paul Pogba kabla ya kumtungua kipa Christian Abbiati katikati ya kipindi cha pili.
Muargentina huyo akashangilia kwa kunyonya chuchu ya vichanga.
0 comments:
Post a Comment