MSHAMBULIAJI Wayne Rooney amefurahia klabu yake Manchester United's kumsajili Radamel Falcao akisema ni mchezaji mzuri, lakini amesema hahofii kupokonywa namba.
Usajili wa Falcao ndio lilikuwa tukio kubwa zaidi katika siku ya kufungwa pazia la usajili, nyota huyo wa Colombia akitua United kwa mkopo wa Pauni Milioni 6 kutoa huduma kikosi cha Louis van Gaal.
Lakini Nahodha huyo wa United na England, Rooney hahofii ujio wa mchezaji huyo kuhusu nafasi yake kikosini humo na anatarajia kucheza naye.
Pozi: Radamel Falcao akiwa ameshika jezi ya Manchester United baada ya kukamilisha uhamisho wake jana
Akizungumza katika Mkutano na Waandishi wa Habari kuelekea mchezo wa kirafiki wa England dhidi ya Norway, Rooney amesema: "Sijui itaathiri vili nafasi yangu, unatakiwa kumuuliza kocha,"alisema Rooney na kuongeza.
"Nafikiri ni usajili mzuri kwa kuwa ni mmoja wa wachezaji bora duniani," .
0 comments:
Post a Comment