• HABARI MPYA

    Sunday, September 21, 2014

    LAMPARD AIPOKONYA TONGE MDOMONI CHELSEA, AIFUNGA MAN CITY KUPATA SARE BILA KUSHANGILIA

    BAO la dakika za lala salaam la Frank Lampard lineipa sare ya 1-1 Manchester City pungufu dhidi ya timu yake ya zamani, Chelsea jioni hii Uwanja wa Etihad.
    Lampard, aliyejiunga na City kwa mkopo kutoka New York City FC baada ya kutemwa na Chelsea mwishoni mwa msimu, hakushangilia baada ya kufunga bao hilo dakika ya 85.
    Andre Schurrle alitangulia kuifungia Chelsea dakika ya 71, muda mfupi baada ya Pablo Zabaleta kutolewa kwa kadi nyekundu baada ya kuonyeshwa kadi ya pili ya njano kwa kucheza rafu. 
    Frank Lampard hakutaka kushangilia baada ya kufungia Manchester City dhidi ya klabu yake ya zamani aliyoichezea kwa miaka 13 

    Man City: Hart, Zabaleta, Kompany, Mangala, Kolarov/Lampard dk78, Milner, Fernandinho/Jesus Navas dk73, Toure, Silva, Dzeko/Sagna dk70, Aguero. 
    Chelsea: Courtois, Ivanovic, Cahill, Terry, Azpilicueta, Fabregas, Matic, Ramires/Schurrle dk63, Willian/Mikel dk63, Hazard na Costa/Drogba dk86.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LAMPARD AIPOKONYA TONGE MDOMONI CHELSEA, AIFUNGA MAN CITY KUPATA SARE BILA KUSHANGILIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top