BEKI Micah Richards amejiunga na Fiorentina kwa mkopo wa muda mrefu wa msimu baada ya West Ham kushindwa kumsajili mchezaji huyo wa Manchester City.
Richards, mwenye umri wa miaka 26, amesaini klabu hiyo ya Serie A baada ya Hammers kushindwa kumlipa mshahara wake wa Pauni 75,000 kwa wiki.
City pia imepata Pauni Milioni 1 ya ada ya mkopo baada ya West Ham kugoma kumnunua mchezaji huyo wakati uhamisho wa Fiorentina ni wa muda ingawa kuna fursa ya kuuziana moja kwa moja beki huyo.
Maisha mapya; Micah Richards ametua Italia kujaribu kufufua makali yake baada ya mambo kumuendea ndivyo sivyo Man City |
Alipowasili: Micah Richards pichani baada ya kuwasili Florence jana asubuhi kukamilisha uhamisho huo wa mkopo
0 comments:
Post a Comment